Misaada ya Kujifunza
Mhubiri


Mhubiri

Kitabu katika Agano la Kale chenye kuonyesha picha ya baadhi ya matatizo makubwa ya maisha.

Mwandishi wa kitabu hiki, ambaye ni Mhubiri, anaandika sehemu kubwa ya kitabu hiki kutokana na mtazamo wa wale ambao wasio na ufahamu wa injili. Anaandika kulingana na hisia za watu wa ulimwengu—ambao ni, wale “walio chini ya jua” (Mh. 1:9). Sehemu kubwa ya kitabu chaonekana kuwa kinyume, na yaonekana kuwa mambo yote ni mabaya (Mh. 9:5, 10). Hii siyo namna ambayo Bwana angetutaka tuyaone maisha, bali ni namna ambayo Mhubiri alivyoona mambo yanavyoonekana kwa wanadamu wasioelimishwa hapa duniani. Sehemu ya kiroho zaidi katika kitabu hiki iko katika milango ya 11 na wa 12, ambamo mwandishi anahitimisha kwamba kitu pekee chenye thamani ya kudumu ni utiifu kwa amri za Mungu.