Misaada ya Kujifunza
Yehova


Yehova

Agano au jina sahihi la Mungu wa Israeli. Maana yake “Mimi Niko wa milele” (Ku. 3:14; Yn. 8:58). Yehova ndiye Yesu Kristo kabla ya kuzaliwa na akaja duniani kama mwana wa Maria (Mos. 3:8; 15:1; 3 Ne. 15:1–5). Kwa kawaida, neno Bwana lionekanapo katika Agano la Kale, linamaanisha “Yehova.”

Yehova ndiye Kristo

Yehova alijulikana kwa manabii wa kale (Ku. 6:3; Ibr. 1:16). Mtume Paulo alifundisha ya kuwa Kristo alikuwa ndiye Yehova wa Agano la Kale (Ku. 17:6; 1 Kor. 10:1–4). Kaka yake Yaredi katika Kitabu cha Mormoni alimwona Kristo kabla ya kuzaliwa na Akamwabudu (Eth. 3:13–15). Moroni pia alimwita Kristo “Yehova” (Moro. 10:34). Katika Hekalu la Kirtland, Joseph Smith na Oliver Cowdery walimwona Yehova mfufuka (M&M 110:3–4).